Quantcast
Channel: Swahili Time
Viewing all 571 articles
Browse latest View live

Rais Mstaafu George H.W. Bush ni Mzima!

$
0
0
Wadau, siku Rais Donald Trump anaapishwa tulidhani kuwa Rais Mstaafu George H. W. Bush, yuko mahututi atakufa dakika yoyote. Mke wa Barbara naye alikuwa hoi hospitalini. Ajabu juzi tuliwaona kwenye mchezo wa Super Bowl, wakitabasamu,kupungia watu na hata kufanya coin toss, kujua nani atarusha mpira kwanza. Wataishi maisha mrefu hao. Sasa watu wanafanya matani !😂😂😂
j


Wasanii Wanaohusishwa na Madawa ya Kulevya Kisutu Court Leo!Ki

Usiharibu Harusi Yako na Make -Up ya Ajabu!

Kinana Akutana na Waziri Mkuu Majaliwa Leo

$
0
0
KINANA AFANYA MAZUNGUMZO NA WAZIRI MKUU MAJALIWA,LEO LUMUMBA JIJINI DAR ES SALAAM
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimpokea Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa, alipowasili katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, leo, Februari 18, 2017, kwa ajili ya mazungumzo baina yao
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwa na Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa, alipowasili katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, leo, Februari 18, 2017, kwa ajili ya mazungumzo baina yao
Wakienda eneo la kufanyia mazungumzo
Wakiwasili eneo la mazungumzo Ofisini kwa Katibu Mkuu wa CCM.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (kulia) akizungumza na Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, leo Feb 18, 2017. (Picha zote na Bashir Nkoromo)

Mbunge Ritta Kabati Kusaidia Ujenzi wa Ofisi Tatu za CCCM Manispaa ya Iringa

$
0
0
MBUNGE wa viti maalumu Mkoa wa Iringa Ritta Kabati kupitia chama cha mapinduzi (CCM) akimkabidhi mifuko ya saruji kwa ajiri ya ujenzi wa jengo la ofisi ya chama katika kata ya Ruaha kwa mwenyekiti wa chama cha mapinduzi(CCM) manispaa ya Iringa Abeid Kiponza
 MBUNGE wa viti maalumu Mkoa wa Iringa Ritta Kabati kupitia chama cha mapinduzi (CCM) akiwa katika eneo la uwanja wa kujenga ofisi ya kata ya Ruaha
 MBUNGE wa viti maalumu Mkoa wa Iringa Ritta Kabati kupitia chama cha mapinduzi (CCM) akibadilishana mawazo na katibu wa ccm manispaa ya Iringa Nuru Ngereja
 MBUNGE wa viti maalumu Mkoa wa Iringa Ritta Kabati kupitia chama cha mapinduzi (CCM) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wanachama wa hama hicho wa kata ya ruaha
 MBUNGE wa viti maalumu Mkoa wa Iringa Ritta Kabati kupitia chama cha mapinduzi (CCM) akiwa na
mwenyekiti wa chama cha mapinduzi(CCM) manispaa ya Iringa Abeid Kiponza pamoja na viongozi wengine wa chama hicho.
 MBUNGE wa viti maalumu Mkoa wa Iringa Ritta Kabati akipokelewa na wanachama wa mtaa wa kigamboni mkoani Iringa

Na Fredy Mgunda,Iringa.

MBUNGE wa viti maalumu Mkoa wa Iringa Ritta Kabati kupitia chama cha mapinduzi (CCM) ameanza kusaidia Ujenzi wa ofisi za Matawi ya CCM katika kata mbali mbali za Jimbo la Iringa mjini kama sehemu ya majukumu yake ya kukijenga chama hicho ambacho kilipoteza kiti cha ubunge na halmashauri kuchukuliwa na wapinzani.

Akizungumza wakati wa kukabidhi mifuko ya saruji kwa Ujenzi wa ofisi za Tawi Kigamboni na Ruaha ,Kabati alisema kuwa anafanya hivyo kama njia ya kutekeleza ilani na maadhimio ya miaka arobaini ya chama cha mapinduzi.
“Nakipenda chama changu ndio maana napigana sana kuhakikisha chama cha mapinduzi mkaoni mhapa iringa kinarudi mahala pake na kuhakikisha kinaaminika kwa wananchi na wanachama wa  manispaa ya Iringa”.alisema Kabati 

Hata hivyo Kabati alisema kuwa ataendelea kusaidia Ujenzi wa ofisi hizo ili kuona ndani ya kipindi kifupi cha miezi mitatu ama sita kila tawi linakuwa na ofisi yake ya tawi na aliwataka wanachama wa CCM kushikamana na kuendelea na Ujenzi wa ofisi hizo pamoja na kujihusisha na shughuli nyingine za kijamii

"Haiwezakani chama kikubwa kama hiki kukosa ofisi za matawi wakati tunamaeneo mengi ya kujenga ofisi nitakikisha tunashirikiana na wanachama na wananchi wengine kujenga hizo ofisi ili kumuunga mkono Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DR John Pombe Magufuli ambaye anapambana kuhakikisha cha mapinduzi kinakuwa chama cha wananchi wa chini na sio matajiri pekee yao".alisema Kabati

Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha mapinduzi(CCM) manispaa ya Iringa Abeid Kiponza aliwataka wanachama kuwa kusahau yaliyopita na kuanza kujenga chama upya.
“Tulipoteza halmashauri ya Iringa na jimbo hivyo inabidi tukae chini na tujipange upya kukijenga chama maana tunajua kwa kujenga ofisi za matawi zitatusaidia kurudisha hadhi na hali ya chama hapa manispaa kwa kutoa huduma bora kwa wananchi wote bila kuchagua chama”.alisema Kiponza 

Kiponza alimshukuru mbunge wa viti maalumu Ritta kabati kwa mchango anaoutoa kwa kuleta maendeleo katika manispaa ya Iringa hasa ukiangalia ujenzi wa majengo mbalimbali ya shule,taasisi za kidini,taasisi za kijamii hapa kujenga majengo ya chama.

Lakini Kiponza alimtaka mbunge Kabati kuwasaidia wananchi wanaodhurumiwa na kunyang’anywa mali zao katika manispaa ya Iringa.

“Hapa kigamboni kunawananchi wanapigwa na viongozi wa mtaa kwa kuwa wapo CCM tu na wamenyang’anywa kituo cha kuchotea maji ambacho kilikuwa mradi wa chama cha mapinduzi hivyo lazima upambane kuhakikisha wananchi wanaishi kwa amani na mali za chama zinarudi kwenye chama”.alisema Kiponza

 Naye Katibu wa CCM manispaa ya Iringa Nuru Ngeleja alisema kuwa wamejipanga kuhakikisha ofisi zote za chama zinajengwa na zinakuwa katika ubora unaotakiwa kutokana na ukubwa wa chama cha mapinduzi(CCM) na kuahidi kuwa wataendelea kumuunga mkoano Rais wa jamhuri ya muungano ya Tanzania Dr John Pombe Magufuri.

“Sisi tunafanyakazi ya kumsaidia mwenyekiti wetu wa chama ambaye ni Rais wetu kwa kufanya kazi na kuisimamia serikali kufanya kazi kwa uhakika na kuwafaikia na kuwatumikia wananchi waliowaweka madarakani mpaka sasa”. Alisema Ngereja

Wachawi Wamloga Rais Trump wa Marekani!

$
0
0
Usiku wa kuamkia leo,  Wachawi duniani waliungana kumloga Rais Donald J, Trump wa Marekani.  Nia yao ilikuwa wamfanyie dawa asiweze kumwumiza mtu.  Tutaona kama walikuwa na mafaniko.

Asante Rais Trump, ubaguzi unashamiri Marekani.  Wahamiaji wanajificha kwa woga, wazungu wabaguzi wanatukana na kupiga weusi na wasio wazungu ovyo. Tumerudi kwenye enzi za Jim Crow.  Weusi wakienda kwenye migahawa kadhaa wanaambiwa kwa vile Trump ni Rais, si lazima wahudumie weusi! Khaa!  Ubaguzi na utawala aliyoleta Trumo inanafana ya yule mshenzi aliyetawala Ujerumani, Adolf Hitler.

Trump ameaapa kuwa mema aliyofanya Rais Obama atafuta.  Mungu atunusuru na Trump!

Kwa habari zaidi BOFYA HAPA:


Mama Salma Kikwete Ateuliwa Kuwa Mbunge Vitu Maalum

Ujumbe wa Polopole Kuellekea Mkutano Mkuu Maalum wa CCM Mjini Dodoma Machi 12, 2017


Liberian Civil War Atrocities

$
0
0
Murder Victims in Liberia Civil War

   MONROVIA, Liberia (AP) - The skeletal remains of 27 people were all that was left of a massacre, one of many in this West African nation's back-to-back civil wars more than a decade ago. When the United Nations handed over the bones to the government last month, it was an invitation to investigate. Instead the remains were buried quickly, without ceremony, in a site intended for victims of the Ebola virus.

   The incident left many Liberians feeling as though the government wanted to bury the past, too.

   As the U.N.'s peacekeeping mission prepares to leave Liberia with the country's return to stability, questions remain about who must take responsibility for the atrocities over 14 years that left some 250,000 dead.

   Unlike neighboring Sierra Leone, which also suffered from the fighting that spilled over the border, Liberia has yet to deal with perpetrators of the killings, many carried out by drugged and under-age fighters, overseen by people who may now be in power.

   "If there is a need for exhumation for further investigation, that will happen," Information Minister Eugene Nagbe told The Associated Press, insisting the remains of the 27 people were not buried in the same spot where victims of the Ebola outbreak were buried.

   The government of President Ellen Johnson Sirleaf, a Nobel Peace Prize winner, has said it is taking measures to reconcile with the past, but human rights advocates say the president doesn't have the political will to allow the pursuit of past crimes. Before she took power, Sirleaf said that if she was elected she would go for reconciliation instead of prosecution.

   Some in Liberia see this year's election as a chance to bring in a government that might take a more assertive approach.

   The bones handed over by the U.N. mission are thought to be those of victims of the River Gee massacre in 2003, which left more than 360 dead, the New Democrat newspaper reported, citing a 2008 report of the truth and reconciliation commission set up after the civil wars. The U.N mission had begun a forensic investigation into the killings but chose to turn over the bones as its gradual withdrawal from Liberia continues. The mission ends in March 2018.

   The truth and reconciliation commission had blamed on forces loyal to former Liberian rebel leader-turned-President Charles Taylor. Taylor is currently serving a 50-year sentence in Britain after being found guilty of war crimes by a U.N.-backed special court for his role in the bloody civil war in Sierra Leone when he was Liberia's leader.

   Liberia has never had such a special court, though the truth and reconciliation commission had recommended criminal prosecution for dozens of ex-warlords and a 30-year political ban for people who supported the war.

   One of those supporters was Sirleaf, who reluctantly appeared before the commission in 2008 and admitted to providing $10,000 to Taylor when his National Patriotic Front rebel movement was fighting the regime of then-President Samuel Doe.

   But Sirleaf told the truth commission that the money to Taylor was for "humanitarian purposes." Her critics have debunked this, saying that in the 1990s Taylor and his rebels weren't pursuing any humanitarian venture. Meanwhile, Sirleaf held a string of overseas positions with the United Nations and the World Bank and returned to Liberia only in 2004 when Taylor was forced to step down. She was elected president the following year.

   The truth and reconciliation commission's recommendations for criminal prosecution and political bans have never been implemented, and many people named by the commission are now senior members of Liberia's government. The National Human Rights Commission, tasked with implementing the commission's suggestions, remains underfunded.

   Meanwhile, many massacres during the fighting from 1989 to 2003 remain uninvestigated, Liberians say. Some prefer to be done with the past, but others feel closure is vital.

   "It is hard and worthless to keep repeating the graphic of the scene and see the hate and vices that occasioned the war still exist unabated," said Isaac Redd, director of press at the House of Representatives who survived a 1994 massacre at Kpolokpai. "I have personally prayed for the lost souls and asked God to take control for the perpetrators. I have forgiven them."

   Redd, a local radio reporter at the time, recalled that "deaths by chopping off limbs and heads with machetes were ordered without discrimination." Victims were tied up on arrest, and there was no interrogation. "Heads were smashed against the rocks in the middle of the town."

   Those rocks still take center stage in the small coffee-growing town. Visitors stand by them, agape, as survivors explain the atrocities.

   Like the rest of the survivors, Redd does not know how many people were killed in the Kpolokpai massacre, but he said that when rebel fighters released him the next morning, "I was confused but remembered seeing around a hundred bodies on the rocks."

   Many have called for the establishment of a war crimes court like the one that existed in post-conflict Sierra Leone, even as some say no amount of accountability can ease the trauma left behind.

   Peterson Sonyah, who witnessed killings in another assault that has come to be known as the Lutheran Church Massacre, is among those calling for a war crimes tribunal "so that our ugly past cannot haunt us as a nation."

   Sonyah survived an attack by Doe's troops by hiding under a church bench. Around him, soldiers opened fire, the flashes brightening the hall as if it was daytime.

   "People started crying all over the place. Women were raped and made to give out whatever money they had to the soldiers before they were gunned down," he said.

   Sonyah said Liberia Massacre Survivors Association has identified 69 mass graves in five of the country's 15 counties in the hope that someone will take interest. None is under investigation by the government.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utallii Yatembela Eneo lenye Mgogoro la Por Tengefu la Loliondo

$
0
0
Msafara wa Magari ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi,Malisili na Utaalii,yakpita katika maeneo mbalimbali ya Pori Tengefu la Loliono kwa ajili ya kujionea hai halisi ya mgogoro ulioo katika eneo hilo.
Mwenyekii wa Kamati ya Kudumu ya Ardhi ,Maliasii na Utalii,Atashasta Ndetiye (katikati) akiongozana na wajumbe wengine wa kamati hiyo kutizama vyanzo vya maji vilivyoko katika Pori Tengefu la Loliondo.
Waziri wa Malisili na Utalii ambaye pia ni mjumbe wa kamati hiyo,Prof Jumanne Maghembe akiongozana na wataalamu katika ziara ya kamati hiyo.
Mtafiti Mkuu wa Idara ya Ikolojia (TAWIRI) Dkt Edward Khoi akitoa maelezo ya kitaalamu kwa wajumbe wa kamati ya kudumu ya Ardhi,Malisili na Utalii wakati wakitembela Pori tengefu la Loliondo.
Baadhi ya wajumbe wa kamato hiyo wakifuatilia maelezo kutoka kwa wataalamu wa Ikolojia na Uhifadhi.
Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti,William Mwakilema akiwaeleza wajumbe w kamati hiyo madhara yatakayojitokea endapo eneo la Pori Tengefu la Loliondo halita hifadhiwa.
Wajumbe wa Kamati ya Maliasili na Utalii,wakitizama eneo linalotajwa kutengenezwa na wafugaji kwa ajili ya kunyweshea maji mifugo yao ndani ya Pori Tengefu la Loliondo.
Eneo linalouiwa na wafugaji unyweshea mifgo yao.
Sehemu ya Mabirik yanayotajwa kutengenezwa na jamii ya wafugaji kwa ajili ya kunywesha mifgo yao.
Mwenyekiti a Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi,Maliasili na Utalii,Atashsta Ndetiye (kulia) pamoja na Waziri wa Malisili na Utalii,Prof ,Jumanne Maghembe wakitizama eneo ambalo i mapiio ya maji katik Pori Tengefu la Loliondo.
Moja ya Makundi ya Ng'ombe yaliyokutwa na Kamati hiyo katika Pori Tengefu la Loliondo.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi,Maliasili na Utalii wakizungumza na mmoja wa wafugaji waliokutwa wakichunga Ngombe ndani ya Pori Tengefu la Loliondo. 
Kamati ilikutana pia na Changamoto ya uboovu wa Miundombinu ya barabara hali iliyolazimu magari kupita kwa tahadhari .
Wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi,Maliasili na Utalii wakitizama moja kati ya vyanzo vy maji vinavyotiririsha maji yake katika mto Gurumeti uliopo katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Mbunge wa Jimbo la Sumve ambaye pia ni mjube wa kamati hiyo,Richard Ndasa akizungumza jambo mara baada ya kutizama moja ya vyanzo vya maji vilivyoko katika eneo la Pori Tengefu la Loliondo.
Sehemu ya Makundi ya Mifugo pamoja na Mashamba yaliyopo katika eneo la Pori Tengefu la Loliondo.


Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,Kanda ya Kaskazinia

Prof. Samahani Kejeri Explains History of his Name

Dk. Ryoba Awaona Waanidshi wa Habari wa Uhuru Leo

$
0
0
DK. AYUB RIOBA AWANOA KWA SEMINA YA WELEDI WAANDISHI WA HABARI WA GAZETI LA UHURU, JIJINI DAR ES SALAAM, LEO
 Mwandishi wa habari nguli wa siku nyingi,Dk. Ayub Ryoba, akiendesha semina ya kunoa weledi wa taaluma ya uandishi wa habari kwa waandishi wa habari na baadhi ya watumishi wa Kampuni ya Uhuru Publications Ltd, Wachapishaji wa Magazeti ya Uhuru, Mzalendo na Burudani, leo katika Ukumbi wa Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam. Dk. Ryoba ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), ana shahada ya Udaktari wa Falsafa (PhD) katika Sayansi ya Jamii aliyoipata katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 Mwandishi wa habari nguli wa siku nyingi,Dk. Ayub Ryoba, akiendelea kutoa 'nondoz' kwa wafanyakazi hao wa UPL, huku wafanyakazi hao wakimsikiliza kwa makini sana
 Mwandishi wa habari nguli wa siku nyingi,Dk. Ayub Ryoba, akifafanua mada zake kwenye semina hiyo ya kunoa weledi wa kitaaluma
 Washiriki wa semina hiyo wakiwa ukumbini
 Dk. Ayub Ryoba, akiendelea kutoa mada kwenye semina hiyo
 Washiriki wakifuatilia kwa makini mafunzo ya Dk. Ryoba
 Yassin Kayombo (aliyesimama) akijitambulisha kwa Ryoba (kulia) na kwa washiriki wengie wa semina hiyo
 Mgaga akijitambulisha
 Jongo akijitambulisha
 Mnkondo akijitambulisha
 Ally akijitambulisha
 Furaha Omari akijitambulisha 
 Gailanga akijitambulisha
 Utambulisho ukiedelea
 Utambulisho ukiendelea
 Washiriki wakiwa ukumbini
 Dk. Ryoba akiendelea na semina hiyo
 Washiriki wakiwa katika kundi la kwanza kujadili mada
 Washiriki katika kundi la pili kujadili mada
 Washiriki katika kundi la tatu kujadili mada
 Washiriki kundi la nne wakijadili mada
 Dk Ryoba akipitiapitia mada zake wakati akisubiri mrejesho wa maswali aliyowapa washiriki 
 Dk. Ryoba akijadiliana jambo na baadhi ya washiriki wa semina hiyo wakati wa mapumziko. Kulia ni Furaha Omar na Bashir Nkoromo
 Dk. Ryoba akijadiliana jambo na baadhi ya washiriki wa semina hiyo wakati wa mapumziko. Kulia ni Furaha Omar na Bashir Nkoromo
(PICHA ZOTE NA KAMERA YA BASHIR NKOROMO)

Mbinu Hizi zitakusaidi Kukabiliana na Mvua Jijini Dar es Salaam

$
0
0
Na Jumia Travel Tanzania

Hivi kuna mkazi yeyote wa jiji la Dar es Salaam ambaye ni mgeni wa adha zitokanazo na mvua zinazonyesha? Sidhani kama kuna mtu yeyote hafahamu ya kwamba mvua ikinyesha kutakuwa na foleni zisizokwisha, barabara na mitaa tofauti jijini kujaa maji, mafuriko na matamko kadha wa kadha kutoka kwa viongozi wa serikali kuwataka wananchi wahame mabondeni.

Lakini ni wangapi wametafakari watawezaje kukabiliana na mvua zitakaponyesha? Zipo mbinu nyingi tu ambazo Jumia Travel inakushauri uzizingatie ili kipindi cha mvua nyingi za Dar es Salaam kwako kiwe ni cha kawaida katika mwaka. 


Amka mapema kukabiliana na foleni ili uwahi shughuli zako
Hakuna wakati ambao kunakuwa na foleni kubwa na zisizopungua kwa muda mrefu jijini Dar es Salaam kama kipindi cha mvua! Lakini jambo hili sio la kushangaza kwa sababu kila mwaka hali hii inajirudia. 

Na hiki ni kipindi ambacho mabosi wengi huchukia sana pengine kuliko vipindi vyote vya mwaka maana visingizio vya wafanyakazi wao kuchekelewa kazini kwa sababu ya mvua huwa haviishi. Kwa hiyo unakabiliana vipi na hali hiyo? 

Kwanza kabisa lazima uwe makini katika kuwahi kuamka mapema na pia njia ya usafiri utakayoitumia. Inakubidi kuwahi kuamka mapema sana kama unategemea usafiri wa umma au binafsi. Kwa sababu ukifanya hivyo kama kutakuwa na foleni barabarani basi utaziwahi ukilinganisha na ukichelewa kuingia barabarani. Lakini pia kama unategemea usafiri wa umma, mabasi ya mwendokasi ni mkombozi mkubwa kwenye kipindi hiki. Hivyo kwa maeneo ambayo usafiri huu unapatikana ni vema kuutumia ipasavyo kwa sababu yenyewe hayakai foleni kutokana na kuwa na njia zao pamoja na kupewa kipaumbele.    

Nunua vifaa vya kujikinga na mvua
Kutokana na jiji la Dar es Salaam kuwa na vipindi virefu vya jua na joto kali, imekuwa ni nadra sana kuwakuta wakazi wake wana vifaa vya kujikinga na mvua kama vile mwamvuli, koti, sweta au viatu vya mvua. Inashauriwa kuwa na vifaa hivi nyumbani kwako ili kujikinga ifikapo kipindi cha mvua na sio kuanza kufikiria kununua kwani inawezekana usiwe na bajeti hiyo pindi unapovihitaji. Vifaa hivyo ni muhimu kwani hukukinga na baridi, kutolawana, magonjwa na hata kutunza mavazi yako kutokana na maji ambayo huweza kusababisha kuharibika.
Umakini kwenye chombo chako cha usafiri 
Kwa wenye vyombo vya usafiri wanajua wenyewe ni kadhia gani wanayokumbana nayo ikifika kipindi cha mvua. Kipindi hiki ni jambo la kawaida kukuta magari kadhaa yamezimika au kukwama barabarani kutokana na sababu mbalimbali za kiufundi. Lakini pia barabara nyingi huharibika na kutopitika kabisa hivyo kulazimisha chombo chako kupita ni kujitafutia kuingia gharama zisizohitajika siku za usoni. Kama inawezekana tafuta njia mbadala ya usafiri katika kipindi hiki au pita kwenye njia ambazo una uhakika ni salama kwa chombo chako.

Kuwa makini na vifaa vyako vya umeme
Siyo vifaa vyote vya umeme vimetengenezwa vikiwa na uwezo wa kuzuia maji kutokuingia ndani yake. Licha ya makapuni mbalimbali kuja na teknolojia hiyo lakini unashauriwa kuwa makini sana aidha kwa kuvivika vifaa maalumu vya kuzuia maji au kuvikinga kabisa na maji. Kipindi hiki ndicho ambacho wengi hupatwa na majanga ya kuharibikiwa na simu, kompyuta, radio pamoja na luninga huko majumbani.

Kuwa makini na vyakula utakavyokula
Kama huwa unakuwa makini na aina ya vyakula unavyokula basi kipindi hiki inabidi uwe makini zaidi. Mvua zikinyesha jijini Dar es Salaam ndiyo kipindi ambacho pia kunakuwa na mlipuko wa magonjwa kadha wa kadha kama vile kipindupindu. Inashauriwa kula chakula sehemu ambayo unaiamini na inayozingatia usafi wa hali ya juu au kama inashindikana uwe unabeba chakula unachopika mwenyewe au kutokula kabisa.  

Tumia muda wako kusoma vitabu
Sio watu wote wana utaratibu wa kusoma vitabu kwenye siku zao za kawaida badala yake wanatazama filamu, kusikiliza muziki, kutoka wikendi au kupendelea kutembea. Lakini katika kipindi hiki ambacho mvua zinanyesha, barabara hazipitiki, hali ya hewa ni baridi na sehemu nyingi za starehe au kutembelea zinakosa watu ni vema ukajaribu kusoma vitabu. Amini usiamini kuwa hata kutazama filamu na kusikiliza muziki hufikia mahala vinachosha, hiki kinaweza kikawa ni kipindi kizuri cha kujaribu kitu tofauti, nunua vitabu na usome ili uongeze maarifa. 

Hivyo basi tusiifanye mvua ikawa ni kisingizio cha kutofanya shughuli zingine au majukumu mengine yanayotukabili. Kila kipindi huja na changamoto pamoja na fursa zake, ni vema kupambana nazo na kuzitumia ili kusonga mbele.

Comfort Zone - A Poem by Prof Richard Mabala

$
0
0
FROM FACEBOOK

Comfort Zone

By Richard Mabala 

First they came for the big guys
They were all fisadis
But I am not a fisadi so why should I speak out?
Even if no evidence has been given against them
We were told they were fisadis
What greater evidence do you want?
Silently I applauded.
Then they came for the artists
Decadent artists leading immoral lives
Why should I support them?
No evidence again but God had spoken
I said not a word.
Of course they came for the gays
Even wanted to publicly declare their names
Even more disgusting than the artists
I don't care whether they do it in private or not
They deserve it.
No need to speak out
They also came for the activists
Those arrogant unelected nobodies
Pushing their own agendas as if they were the people's choice
They had to be silenced
So silent I remained.
Then they came for an Asian
These Asians, don't we know them
They are just exploiting us
How can he claim to be a citizen like me?
A proud Tanzanian
So what if he was a councillor in my own party
Why should I speak for these exploiters?
And anyway I support that other team
Too patriotic to support him or his team.
So no need to speak out
Even if there seems be a vendetta against him
For daring to threaten the son of God
Silence is golden
Then they came for the opposition.
Why should they go on politicking even after the election.
Throw them in jail
And keep them there to show our leaders brook no opposition
Opposition disrupts their good intentions.
Troublemakers.
They deserve to stay in jail
I said nothing
The same is true of those people
Who used unbecoming language
On Facebook
They should have known better
They were warned
But still the persisted.
Why should I speak in their favour
Then they came for the lawyers
Especially those dumb oppositionist lawyers
Wanting to take over their association
And become activist
Activist? Really?
We know those lawyers are just after money
And power
Corrupt.
Surely they can defend themselves anyway.
Say nothing.
Then they came for their own party members
Ha ha ha. You see their foolishness
Fraternising with the enemy when politics is no longer about adversaries
But enemies.
They couldn't even see which way the wind is blowing
And bow before it
They were flattened
And I will never say a word
Even if they belonged to my party
Unlike them, I am loyal
Always loyal.
But hang on
What are those boots outside my door?
What have I done?
HELP! Will someone speak out for me?
I have done nothing.
Why the silence?
Am I the only one left?

Uzinduzi wa WASATU - Northampton, Uingereza

$
0
0
PICHA ZA HABARI : UZINDUZI WA WASATU NORTHAMPTON , UINGEREZA

Na Freddy Macha 

 Jumuiya ya wasanii Watanzania Uingereza (WASATU) ilizunduliwa kwa vigelegele na muziki mjini Northampton , katikati ya Uingereza jumamosi iliyopita. Tafrija hiyo ndogo lakini iliyowakutanisha zaidi ya Watanzania mia moja na  wenzao wa Kenya, Uganda, Kongo , Nigeria, Uingereza nk, ilihudhuriwa na Mheshimiwa Balozi Dk Asha Rose Migiro.
 

WASATU ilibuniwa mwaka jana kati ya wasanii wakiongozwa na mwanamuziki na mcheza sarakasi Fab Moses na promota wa vyakula vya Kitanzania, Bi Neema Kitilya. Asilimia 20 ya kipato cha onesho zilitolewa na WASATU kwa walio Northampton; kwa maafa ya mafuriko ya maji karibuni Tanzania. 

Pichani: Watanzania na wasanii wenzao wakijimwaga ukumbi wa The Eastern District Social Club, Northampton











Furaha na shangwe ya WASATUBalozi Migiro (katikati) na mwana WASATU- mcheza ngoma asilia, Khadija Ismail. Wa kwanza ni Mtanzania, Salma KashindeMuziki motomoto, NorthamptonBango la shughuliBalozi Migiro akihutubia tafrijaMpiga sasafoni mkongwe na mwanaWASATU- RamaSax- mzawa wa Tanga akipuliza vituzWASATU. Toka kushoto nyuma, Rama Sax, Saidi Kanda, John Londo, Fab Moses , Freddy MachaMbele : Khadija Ismail na Neema Kitilya. Picha na ShahVitumbua vya Neema KitilyaNyama ChomaMwana WASATU Fab Moses akionesha vituko vyake vya SarakasiMwanamuziki wa Kikongo aliyehamia Tanzania miaka mingi, Kawele Mutimanwa na bendi ya “Afrika Jambo” jukwaani NorthamptonMwanamuziki mlemavu na msanifu picha, Kea , toka Kenya aliyetengeneza tangazo la WASATU Mwanamuziki wa Kikongo Mboka Lia ( anayejulikana kwa jina “Burkina Faso”) ndani ya nyuzi na sakata sakata la WASATU Mwanamuziki mlemavu aliyekomaa- mtunzi, mwimbaji na mpiga gitaa hatari, John Londo – mwana WASATU aliyebobea. Kileleni Northampton bila kukosa.

Kuwanasa Wauji wa Albino, Mbinu za Kivita Zinatumika!

$
0
0

Mwandishi wa makala haya na mmiliki wa blogu ya MaendeleoVijijini, Bw. Daniel Mbega (mwenye jezi nyekundu) akiwa sambamba na wanausalama katika tukio la kukatwa kiganja mtoto Baraka Cosmas Songoloka. Hapa ni kwenye tukio katika Kitongoji cha Kaoze, Kilyamatundu wilayani Sumbawanga.

Na Daniel Mbega, MaendeleoVijijini
Tabora: KWA wakazi wa Kitongoji cha Kona Nne, Kijiji cha Ugembe II, Kata ya Mwakashanhala wilayani Nzega katika Mkoa wa Tabora, takriban kilometa 90 kutoka Nzega mjini, saa 3:00 ni usiku mkubwa na wengi wamelala baada ya shughuli za ujenzi wa taifa.

Majira kama hayo, usiku wa Jumatatu, Juni 15, 2015 haukuwa na tofauti kubwa, isipokuwa giza lililotanda kutokana na mbalamwezi kuwa gizani.
Kama ilivyo kwa maeneo mengi ya vijijini ambako watu hulala mapema, sauti pekee zinazosikika majira hayo ni ng’ombe wakilia na mahali pengine mlevi mmoja akiimba nyimbo katika lugha ya Kinyamwezi ambazo hazina mpangilio maalum wakati akirejea kutoka kilabuni.
  Mwandishi wa makala haya na mmiliki wa blogu ya MaendeleoVijijini, Bw. Daniel Mbega akiwa na Margreth (kushoto) na kaka yake, Tano baada ya wanausalama kufanikiwa kumnusuru binti huyo aliyetekwa na mjomba wake asiweze kwenda kuuzwa katika Kitongoji cha Kona Nne, Kijiji cha Mwakashanhala wilayani Nzega.

Mwandishi wa makala haya, akiwa katika harakati za kufanya uchunguzi kuhusu mauaji ya albino, alijikaza kisabuni huku akiugulia maumivu ya mbigili zilizomchoma magotini wakati akiwa amejificha kwenye kichaka pamoja na askari wawili wenye bunduki.
Mmoja wa askari hao alikuwa na bunduki aina ya Sub-Machine Gun (SMG) ambayo alizibana magazine mbili kwa pamoja, na mwingine akiwa na bunduki ya mabomu ya machozi (Anti-Riot Gun) huku akiwa ameyapachika mabomu ya kutosha kiunoni mwake, ikiwa ni tahadhari endapo fujo zingetokea.
Silaha pekee ya mwandishi ilikuwa kalamu na daftari dogo la kuandika kumbukumbu pamoja na simu kubwa ambayo aliitumia kama kamera tu kwa sababu sehemu hiyo mtandao haupatikani.
Zoezi hili la kivita lilikuwa na lengo moja tu la kumnasa mtu aliyedaiwa kutaka kumteka nyara mtu mwenye albinism na kwenda kumuuza ili apate utajiri.
Mwandishi, ambaye alikwishazunguka kwa karibu miezi sita wakati huo kuchunguza mauaji ya albino akiongozana na vikosi vya usalama, alikuwa anataka kushuhudia kwa macho yake ili kukamilisha uchunguzi huo na kuandika ukweli wa matukio ya mauaji ya albino ambayo yameshamiri nchini Tanzania na Afrika Mashariki na Kati tangu yalipoibuka kwa kasi mwaka 2006.
Nyumba pekee ya jirani ilikuwa umbali wa takriban meta 120 kutoka mahali walikojificha, ambayo ndiyo nyumba ya tukio.
Lakini umbali wa meta 10 kutoka walikojificha kulikuwa na njiapanda ambako liliegeshwa gari aina ya Toyota Land Cruiser Prado Hard Top jeusi ambalo pia lilikuwa na askari kanzu wanne wenye silaha, mmojawao akiwa mwanamke.
“Tulia wewe, ninyi si mmezowea kuripoti habari juu juu na kuona matukio mengine kama ya kutungwa? Mnatulaumu polisi hatufanyi kazi,” mmoja wa askari hao akamwambia mwandishi kwa sauti kali ya kunong’ona baada ya kuona anahangaika kutafuta sehemu salama isiyo na mbigili ambazo ni nyingi katika eneo hili.
Hii haikuwa mara ya kwanza kwa mwandishi huyu kufanya kazi katika mazingira hatarishi katika uchunguzi wa mauaji ya albino, kwani kwa kipindi cha miezi mitano nyuma alikuwa amepenya na kushuhudia operesheni hizo za kipolisi kuwasaka watuhumiwa usiku na mchana na kunusurika hatari mbalimbali.
Mwandishi wa makala haya na mmiliki wa blogu ya MaendeleoVijijini, Bw. Daniel Mbega akiangalia mfupa unaodhaniwa kuwa wa binadamu katika Kijiji cha Bulumbela wilayani Igunga.

Wakati fulani, akiwa na polisi wa kike mkoani Simiyu, waliwahi kuzingirwa usiku kwenye baa na wananchi wenye mapanga baada ya askari waliyeongozana naye kumkamata, bila kuwataarifu, mtu aliyehusishwa na utekaji nyara wa mtoto Pendo Emmanuel Nundi wa Kijiji cha Ndamhi wilayani Kwimba katika Mkoa wa Mwanza. Jinsi walivyonusurika, ni habari nyingine ambayo haina nafasi hapa.
Kusafiri usiku na mchana kwa siku tano mfululizo bila kupumzika lilikuwa jambo la kawaida, na mara kadhaa walinusurika ajali kutokana na uchovu na usingizi.
Pamoja na ujasiri aliokuwa nao, lakini kwa mazingira aliyokuwepo usiku huo, alishikwa na hofu kwa sababu hakukuwepo na mtandao wowote wa simu na barabara pekee kutoka hapo hadi barabara kuu ya Nzega-Tabora, umbali wa kilometa 35, ikiwa ni njia ya ng’ombe.
Kwamba hata kama polisi walikuwa na silaha, lakini kama ingetokea mwano (yowe) ukapigwa na wakazi hao wa jamii ya Wasukuma na Wanyamwezi, hata silaha zenyewe zingeweza kuwa hatarini kwa sababu kusingekuwa na uwezekano wa kupambana na kundi la watu ambao wanaweza kuwadhania wao ni majambazi.
Tukio la kuuawa kwa watafiti watano mkoani Dodoma mwaka 2016 walipopigiwa yowe na wananchi wakidaiwa ni ‘wanyonya damu’, ni mfano mzuri kwamba lolote linaweza kutokea unapokuwa kwenye operesheni za aina hiyo.
Ghafla akatokea mtu mmoja akikimbia kuelekea lilikoegeshwa gari huku akiwa amembeba mtu begani kwake, ambapo mwandishi akainuka kijeshi baada ya kuona askari wale wameinuka na kwenda haraka, lakini kwa tahadhari, liliko gari.
“Upo chini ya ulinzi!” Sauti kali kutoka kwa mmoja wa askari waliokuwa kwenye gari ilisema, huku akiwa nyuma ya mtuhumiwa ambaye tayari alikuwa amemkabidhi mtoto mwenye albinism kwa askari kanzu wa kike aliyekuwa ndani ya gari na mtuhumiwa akavishwa pingu.
Ni wakati huo ambapo mtoto huyo, Margreth Hamisi (6) alizinduka kutoka usingizini kwani mtuhumiwa alikuwa ameingia ndani na kumkwapua na kukimbia naye wakati mama wa binti huyo, ambaye naye ni albino, alikuwa anaota moto nje kwenye kikome.
Mshangao ulimpata mtuhumiwa huyo ambaye alikuwa ameaminishwa na mtu aliyejiita ‘mganga’ kuwa baada ya kuoga dawa aina ya giti (neno la Kisukuma likimaanisha ‘giza’) basi ‘angepotea’ mara atakapomfikisha mtoto huyo kwenye gari na kupewa mamilioni ya fedha kutoka kwa ‘tajiri’ ili akaishi jijini Mwanza.
Naam. Hivi ndivyo mwandishi alivyoshuhudia kwa macho yake namna maofisa usalama walivyofanikiwa kuweka mtego na kumnasa mtuhumiwa Masanja Mwinamila (44), mkazi wa Kitongoji cha Kona Nne, ambaye alitaka kumuuza hai binti wa dada yake kwa mamilioni ya fedha.
“Matukio mengi ya kuuawa au kujeruhiwa kwa watu wenye albinism yanapangwa na kufanikishwa na wanandugu wenyewe kwa sababu ya mawazo potofu ya kutafuta utajiri kwa njia za mkato,” kachero mmoja mwenye cheo cha Sajini Meja (D/SSGT), Mkwabi alimweleza mwandishi wa makala haya.
“Nina uzoefu wa kutosha, miaka 35 ninafanya upelelezi na tangu mauaji ya albino yalipoibuka, kila tukio lazima tu utakuta ndugu anahusika,” akaongeza askari huo akizungumzia uzoefu wake.
Hii ilikuwa ni mara ya tatu kwa wanausalama hao kwenda kijijini kwa nia ya kumkamata mtuhumiwa, lakini mara mbili ilishindikana kutokana na sababu mbalimbali za kiusalama.
Tukio hilo lilitokea takriban wiki tatu baada ya wanausalama kuwakamata watuhumiwa sita Mei 21, 2015 huko Kahama wakiwa katika harakati za kuuza mifupa inayodhaniwa kuwa ni ya watu wenye albinism kwa mamilioni ya fedha.
“Nadhani umeshuhudia, haikuwa kazi rahisi kumwokoa binti huyu akiwa hai na kumtia mbaroni mtuhumiwa, tulilazimika kujifanya ‘wanunuzi’ na ‘waganga’ ili kuweka mtego wa kumkamata na kumwokoa mateka,” akadokeza kachero D/SGT Kato, mmoja wa maofisa ambaye alikuwa kwenye operesheni hiyo.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora wa wakati huo, ACP. Juma Bwire, akitoa ripoti ya tukio hilo, alisema mtuhumiwa Masanja Mwinamila alithubutu kumnyakua mtoto Margret (6) majira ya saa 3 usiku na kukimbia naye gizani akiwa na lengo la kumuuza ajipatie utajiri.
Vyanzo vya habari vilieleza kwamba, mtuhumiwa huyo alianza mchakato wa kutafuta ‘soko’ la kumuuza binti huyo mapema mwezi Juni 2015, lakini wasamaria wema wakawaarifu wanausalama kuhusu kilichotaka kutokea katika eneo hilo.
“Alisema kuna dada yake mwenye albinism ambaye ana watoto wawili – wa kiume na wa kike – ambao nao wana albinism, huyo dada ni mtoto wa baba yake mdogo ambaye alifariki mwaka 2014, hivyo nyumbani hakuna mtu wa kiume wa kuleta upinzani.
“Akasema biashara hiyo ingefanyika sana, kwani alipanga kuanza kumuuza mtoto wa kike, halafu angemuuza yule wa kiume na hatimaye kummalizia dada yake!” kilisema chanzo cha ndani kutoka eneo la tukio.
Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa makala haya umebaini kwamba, asilimia kubwa ya wakazi wa Kanda ya Ziwa ni wapagani na wanawaamini waganga wa jadi kuliko mtu yeyote, hivyo Masanja aliamini kila alichoambiwa na ‘mganga’ feki.
Mganga huyo feki, mbali ya kumpigia ramli na kumwogesha dawa kwenye njiapanda mchana wa jua kali, alimtaka mtuhumiwa kumleta mtoto huyo akiwa hai kwa maelezo kwamba inabidi ‘afanye tambiko ili dawa zifanye kazi’, lakini lengo likiwa kumzuia asimdhuru mateka na hivyo kupata nafasi ya kumwokoa.
Akiwa na shauku ya kupata utajiri na kuachana na umaskini, baada ya kukubali masharti ya mganga, Masanja alimuomba ‘tajiri’ atafute bunduki ili wakati yeye atakapomnyakua mtoto, wafyatue risasi hewani kuwatisha watu watakaokimbilia eneo la tukio ikiwa yowe litakapigwa.
“Kauli hii iliwatisha wanausalama na wakahisi mtuhumiwa angeweza kwenda kuwadhuru watu wengine hata kwa panga ili amchukue mtoto, hivyo mganga akatoa masharti kuwa hata kama bunduki itapatikana, lakini asingependa kuona damu inamwagika kwa yeyote, na akamhakikishia kuwa dawa atakazoogeshwa zitamfanya awe ‘kiza’ asionekane na mtu yeyote,” alifafanua mmoja wa maofisa wa polisi ambaye hakutaka kutajwa jina lake kwa vile siyo msemaji wa Jeshi la Polisi.
Inaelezwa kwamba, mtuhumiwa huyo alipewa masharti mtoto huyo afikishwe kwa mganga akiwa hai bila kujeruhiwa, familia itakayovamiwa pia isimwage damu, fedha za manunuzi kabla ya kukabidhiwa mlengwa lazima zifanyiwe tambiko na masharti ya matumizi, na hakutakiwa kufanya ngono siku nne kabla ya tukio.
Bi. Joyce Mwandu Nkimbui (33), ambaye ni mama wa Margret, alisema siku tatu mfululizo kabla ya tukio, kaka yake huyo anayeishi jirani na hapo alikuwa akija asubuhi na jioni akijifanya kusalimia na wakati mwingine hata kupikiwa chakula.
Hata hivyo, alishangaa kumuona ndiye aliyevamia nyumbani kwao usiku huo na kumwamuru asikimbie kabla ya kuingia ndani na kumkwapua mtoto.
“Walikuja usiku, sijui walikuwa wangapi, lakini wakanilazimisha ‘wewe mama tulia’, nikaogopa na kukimbilia kwenye majani, nikaanguka kwa sababu sioni vizuri usiku, nikakutana na mwenyekiti wa kitongoji, ambaye tulikwenda naye nyumbani na kukuta tayari mtoto hayupo,” Joyce alisema kwa masikitiko.
Wakati tukio hilo linatokea, tayari watu sita walikuwa wamefikishwa mahakamani Juni 3, 2015 na wengine watatu wakisubiri kuunganishwa katika kesi mbili za kujaribu kuua kwa kumkata mkono Bi. Mungu Masaga Gedi, mkazi wa Kitongoji cha Mkuyuni, Kijiji cha Buhekela, Kata ya Igoweko wilayani Igunga, na lingine la kumkata mkono mtoto Nkamba Ezekiel kwenye Kijiji cha Mwisole, Kata ya Lutende, wilayani Uyui.
Katika mahojiano na polisi, watu hao walikiri kuhusika na mauaji ya Mapambo Mashili katika Kitongoji cha Mkuyuni, Kijiji cha Buhekela wilayani Igunga yaliyotokea Agosti 16, 2014, ingawa kesi hiyo ya mauaji bado inaendelea kupelelezwa.
Taarifa za kipolisi zinasema, watu hao walimshambulia kwa mapanga Mapambo Mashili na kumuua wakati akipambana kuzuia mkewe, Mungu Gedi ambaye ana albinism asikatwe mkono.
Hata hivyo, taarifa za kipolisi zinasema, baada ya kumuua Mapambo, watu hao walimkata mkono wa kulia mama huyo na kutoweka nao.
Watu watano kati yao walikamatwa mjini Kahama Mei 22, 2015 wakiwa katika harakati za kuuza mifupa hiyo kwa mamilioni ya fedha.
Waliokamatwa wakati huo ni Bahati Kirungu Maziku (57), ambaye ni mwalimu wa shule ya msingi Mbutu wilayani Kahama, Elizabeth Makandi Sweya Masanja (43) mkazi wa Bungwa wilayani Nzega, Bilia Masanja (39), mkazi wa Bukene wilayani Nzega, Muhoja John maarufu kama Juma (29), mkazi wa Nyasa na Regina Kashinje (41), mkazi wa Isagenhe.
Mei 23, 2015 Polisi walifanikiwa kumkamata Mussa Njile Masanilo (31), mkazi wa Mmale, wilayani Uyui ambaye baada ya mahojiano alikiri kuhusika na matukio hayo na kuwataja washirika wengine ambao bado wanaendelea kusakwa polisi.
Katika mwendelezo wa upelelezi wa tukio hilo, polisi walifanikiwa pia kuwakamata watuhumiwa wengine watatu ambao ni Athumani Masoud Mohammed (56), diwani mstaafu na mkazi wa Kijiji cha Mbutu wilayani Igunga, Bi. Misuka Giti Malisha (51) mganga wa jadi ambaye ni maarufu kama Mwanagiti, mkazi wa Kitongoji cha Mwaningho, Kijiji cha Bulumbela, Kata ya Ziba wilayani Igunga pamoja na Omary Hussein Mkoma (28), mkazi wa Kijiji cha Buhekela wilayani Igunga.
Watuhumiwa hao walihusishwa na washirika wengine sita katika shauri hilo, na inaelezwa kwamba walikiri kushirikiana nao katika biashara mbalimbali ingawa walikana kuhusika na tukio la kukatwa mkono kwa Mungu Gedi na mauaji ya mumewe ingawa walikuwepo kijijini wakati matukio hayo yanatokea.
Kukamatwa kwa Masanja Juni 15, 2015 akitaka kumuuza hai binti wa dada yake kwa mamilioni ya fedha kumedhihirisha kwamba matukio mengi ya kuuawa au kujeruhiwa kwa watu wenye albinism yanapangwa na kufanikishwa na wanandugu wenyewe kwa sababu ya mawazo potofu ya kutafuta utajiri kwa njia za mkato.
Mwaka 2009, Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliangua kilio bungeni kuonyesha uchungu alionao dhidi ya vitendo vya mauaji ya kikatili ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino), na machozi yake yakayeyusha hoja ya wabunge wa upinzani waliokuwa wamepania kumbana, ili ajiuzulu kwa madai kwamba, alitoa amri ya kuua wauaji ambayo ni kinyume na Katiba ya nchi.

Kanda ya Ziwa balaa
Taarifa za kichunguzi zinaonyesha kwamba, mikoa ya Mwanza na Kagera ndiyo vinara wa matukio ya mauaji na kushambuliwa kwa albino nchini tangu kuripotiwa kwa tukio la kwanza dhidi ya walemavu hao lililohusisha mauaji ya Arip Amon, mkazi wa Kijiji cha Nyehunge wilayani Sengerema katika Mkoa wa Mwanza.
Tukio hilo, ambalo mpaka sasa hakuna hata mtuhumiwa mmoja aliyekamatwa, lilitokea Jumatatu, Aprili 17, 2006 majira ya saa sita usiku katika Kijiji cha Nyehunge na lilipewa jalada lenye kumbukumbu namba KAH/IR/92/206.
 Takwimu za kipolisi zinaonyesha kwamba, Mkoa wa Mwanza ndio unaoongoza kwa matukio 12 ukifuatiwa na Kagera wenye matukio tisa (9).
Kwa mujibu wa takwimu hizo, mkoa unaofuatia kwa idadi ya matukio ni Geita ambao mpaka sasa jumla ya matukio sita yametokea wakati Tabora una matukio matano, Kigoma matukio manne, Mara, Rukwa, Shinyanga na Simiyu matukio matatu kila mmoja na tukio moja moja limetokea katika mikoa ya Mbeya, Katavi, Pwani na Tanga.
Inaelezwa kwamba, tangu mwaka 2006 serikali kupitia Jeshi la Polisi imekuwa ikifanya kazi usiku na mchana kupambana na matukio ya kuuawa na kujeruhiwa kwa watu wenye albinism nchini.
Jumla ya matukio 53 yametokea na idadi kama hiyo ya kesi zimefikishwa mahakamani tangu mwaka 2006 hadi 2015 ambayo yamehusisha mauaji, kujeruhi na kuteka nyara na katika kipindi hicho walemavu wa ngozi (albino) 39 waliuawa, 12 walijeruhiwa na wawili walitekwa nyara.
Kati ya waliotekwa nyara, mmoja aliokolewa na Jeshi la Polisi na mtuhumiwa aliyehusika na utekaji huo alihukumiwa kifungo cha miaka 10 jela, tukio ambalo lilitokea wilayani Nzega Juni 15, 2015.
Uchunguzi unaonyesha kwamba, kesi 22 kati ya 53 zimeondolewa mahakamani na watuhumiwa 73 waliachiliwa huru na mahakama na vyombo vingine vya sheria baada ya kuonekana hawana mashtaka ya kujibu.
Aidha, washtakiwa 24 wamehukumiwa kunyongwa mpaka kufa katika mahakama mbalimbali nchini, wakati wawili walihukumiwa vifungo tofauti jela.
Katika Shauri la kujaribu kumuua Emmanuel Festo Rutema (14) wa Isebya – Kagoma wilayani Biharamulo lililotokea Novemba 12, 2007 ambalo lilikuwa na majalada yenye kumbukumbu namba BI/IR/1262/2007 na PI 68/2007 mshtakiwa Zacharia Petro alihukumiwa kifungo cha miaka 20 jela.
Ijumaa Juni 19, 2015 Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Nzega, Saraphine Nsasa, alimhukumu kifungo cha miaka 10 jela mshtakiwa Masanja Mwinamila (44), mkazi wa Kitongoji cha Kona Nne, Kijiji cha Ugembe II, Kata ya Mwakashanhala, Tarafa ya Puge wilayani Nzega katika Mkoa wa Tabora baada ya kukiri kumteka nyara mtoto wa dada yake, Margret Hamisi (6) kwa lengo la kwenda kumuuza mzima mzima.
Katika kesi hiyo NZ/IR/807/2015 yenye kumbukumbu CC. NO. 116/2015, Masanja baada ya kusomewa mashtaka hakuisumbua mahakama pale alipokiri kutenda kosa hilo hasa kwa kuzingatia kwamba ushahidi ulikuwa umekamilika.
Fuatilia mfululizo wa ripoti hii maalum: ‘Unaweza kufukua kaburi la Nyerere?’.

+255 656 331974

Kenyan Doctor Discovers Hepatitis C Treatment

$
0
0

AJABU LIVE VIDEO INTERVIEW: How Kenya’s Dr. Njoroge Discovered HEP C Treatment Drug

(AJABU AFRICA NEWS, APRIL 27, 2017) BOSTON--By leading a team that discovered Victrelis, the first ever effective Hepatitis C treatment drug , in addition to being the first African ever to be granted over 100 patents in the USA, Kenyan born Dr. George Njoroge has continued to be a trail blazer in the bio chemistry arena. 
He has therefore become a great role model for many Kenyans and Africans everywhere who now see living proof that they have what it takes to be competitive on the global arena and rise to the top.

According to the Centers for Disease Control and Prevention (CDC)Hepatitis C kills more Americans every year more than any other infection diseases, with about 19,659 deaths reported in 2014 alone, mainly attributed to low levels of diagnosis and treatment as most patients do not even know they are suffering.

In addition, about 3.5 million Americans are currently living with the disease, with nearly half of them unaware since hepatitis C has no obvious symptoms.

The numbers of deaths and those living with the disease are much higher if the entire world population is taken into account. READ MORE & WATCH VIDEO HERE >>>

Poetry Night in Dar es Salaam

Buriani Mwanahabari Revocatus Bulizya

$
0
0
Marehemu Revocatus Bulizya enzi za uhai wake
Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa Mwanahabari Revocatus Bulizya wakati ukiingizwa katika Kanisa la Katoliki Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya ibada ya kuuaga kabla ya kwenda kwenye mazishi yaliyofanyika Mwandege Kongowe Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam leo.
Mjane wa marehemu na mtoto wao (katikati), akisaidiwa na dada yake aliyewahi kuwa Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Mkoa wa Dar es Salaam toka mwaka 2010/2015, Shelymar Kweygia kuingia katika kanisa hilo kwa ajili ya ibada ya kuuaga mwili huo.



Jeneza likiingizwa kanisani.


Waombolezaji wakiwa katika ibada ya kuuaga mwili huo.
Wanahabari wa Sahara Media alikokuwa akifanya kazi marehemu katika Kituo cha Televisheni cha Star TV na ndugu jamaa wa marehemu wakiwa kwenye ibada hiyo. 
Wanahabari wakiandika wasifu wa marehemu Revocatus Bulizya.
Wanahabari Kibwana Dachi (kulia) na Ben Mwanantala 
wakiwa kwenye ibada hiyo.
Katekista wa Parokia ya Muhimbili akiongoza ibada hiyo.
Ni huzuni katika ibada hiyo.

Na Dotto Mwaibale

VILIO na majonzi vilitawala wakati wa ibada ya kuuaga mwili wa mwanahabari Revocatus Bulizya wa Kituo cha Televisheni cha Star TV wakati wa ibada ya kumuaga iliyofanyika Kanisa Katoliki la Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) Dar es Salaam leo asubuhi.

Ibada hiyo ilihudhuriwa na ndugu jamaa na marafiki wa marehemu pamoja na wanahabari kutoka vyombo mbalimbali akiwepo aliyewahi kuwa Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Mkoa wa Dar es Salaam toka mwaka 2010/2015, Shelymar Kweygia ambaye ni ndugu ya mke wa Bulizya.

Akitoa mahubiri wakati wa ibada hiyo Katekista wa Paroko ya Kanisa Katoliki MNH, alisema ni wakati wa kila mmoja wetu kutafakari juu ya maisha yake ya kimungu.

Alisema hakuna njia ya kukutana na mungu bila ya kifo na ndio maana wakati wote tunatakiwa kujiandaa kwa sababu hatui ni lina tutatoweka duniani kama alivyotuacha ndugu yetu Revocatus Bulizya.

Recocatus Bulizya alzaliwa tarehe 29-10-1979 na kufariki dunia tarehe 2-5-2017 kwa kugongwa na pikipiki 'bodaboda' maeneo ya Pugu jijini Dar es Salaam wakati akirejea nyumbani kwake akiwa ameongoza na mke wake.

Mazishi ya marehemu yamefanyika Mwandege Kongowe Barabara ya Kilwa nje kidogo ya jijini Dar es Salaam na mungu ailaze mahali pema peponi roho ya marehemu.


Tanzia - Mh, Said Thabith Mwambungu

$
0
0
 
The late Regional Commissioner Said Thabith Mwambungu
 
Kutoka kwa mwandishi mahili  Nickson Mkilanya 
 
 KWAHERI YA KUONANA RC SAID THABITH MWAMBUNGU
 
Amefariki leo katika hospitali ya taifa ya muhimbili,hatunaye tena, Said Thabith Mwambungu mkuu wa mkoa mstaaf na miongoni mwa wanasiasa wabobezi na wakongwe katika zama hizi.
Ameripotiwa kusumbuliwa na ugonjwa wa figo kwa siku kadhaa hata akapelekwa kutibiwa nchini India na kurejea na nafuu ambayo pia haikupata kumrejesha katika majukwaa ya siasa na hata hadharani.
 
Kuugua huko pasipo kutajwa kuwa ndiyo sababu iliyopelekea rais Magufuli kumhamishia ofisi ya waziri mkuu na kuahidi kumpangia kazi zingine toka juni 26 mwaka jana lakini nafsi yangu yakiri kuwa pengine hiyo ndiyo sababu kuu.
 
Alilitamka kwa ufasaha jina lake la said said thabith mwangu enzi za uhai wake hasa pale nilipofanyakazi naye mimi nikiwa kama mwanahabari wa luninga,radio na hata magazeti, ni mzaliwa wa Malinyi mkoani Morogoro ambaye kwangu mimi ni miongoni mwa wanasiasa bora,baba Bora na kielelezo cha watu wema na wastaarabu niliopata kukutana nao.

Miongoni mwa mambo aliyoyaacha km funzo kwangu ni uvumilivu na upendo. Wakati mmoja akiwa mkuu wa wilaya kuna kiongozi mmoja alimfanyia figisu figisu nyingi ambazo hata wanahabari tuliona na kugundua akionewa dhahiri! Lakini tulipoongea naye jibu lake alijibu kuwa mwacheni tu huyo, hayo ni yakupita, hajui siasa, vumilieni yataisha na kweli huyo mtu alikuja ondolewa ktk nafasi na kumwacha mwambungu akitamba na siku chache baadae kuteuliwa kuwa mkuu wa mkoa wa ruvuma.
 
Jambo lingine alijua kuthamini watu na kuwaonesha upendo wa dhati hata wale ambao kwa tabia za kibaguzi wasingepaswa kumsogelea lkn bado aliwapa nafasi sawa na wale ambao kimtazamo walikuwa na sifa ya kumsogelea. Nakumbuka wakati mmoja aliniambia nick mwanangu fanya mpango uoe nikufanyie sherehe kabla sijaondoka na hapa alimaanisha kabla hajahamishwa kituo cha kazi nami nilicheka na kuahidi kufanya hivyo lkn leo hatunae tena ameondoka mwambungu pasipo kushughudia harusi yangu.
 
Amini mungu ni mwema wanae wakiongozwa na hamidu mwambungu watashughudia harusi yangu kwa niaba yake inshallah.
 
Wakati wa uhai wake alipata kuwa kada mwandamizi katika ccm, katibu wa chama cha mampinduzi mkoa,  mkuu wa wilaya na mkuu wa mkoa achilia mbali nafasi zingine nyeti ndani ya nchi hii, Na ameacha watoto watatu, hamidu said said thabith mwambungu, Khalid na Abiba S. S Thabith mwambungu na mjane.
 
 Mtoto mkubwa wa marehemu  aitwae Hamidu Mwambungu anasema haijaamuliwa bado kama baba yao atazikwa morogoro au kwingineko.
 
Tangulia mtu mwema Said Said Thabith Mwambungu.
Viewing all 571 articles
Browse latest View live